Burudani

AY kuachia ngoma 2 za kimataifa ukiwemo aliomshirikisha Sean Kingston

AY anatarajia kuachia nyimbo mbili za kimataifa mwezi November mwaka huu. Miongoni mwa nyimbo hizo ni pamoja na ule aliomshirikisha Sean Kingston.

926569_1457488691204165_749843811_n

Akiongea na kituo cha redio cha Nuru FM cha Iringa hivi karibuni, AY alisema miezi ya hivi karibuni amekuwa akiachia nyimbo kwaajili ya soko la ndani ukiwemo ‘Asante’ na wimbo mwingine atakaoutoa hivi karibuni. Alidai kuwa baada ya nyimbo hizo ndipo atakaporejea tena kwenye nyimbo kwaajili ya soko la kimataifa.

Katika hatua nyingine AY amekiambia kituo hicho kuwa yeye na Diamond watawekeza kufanya video ya wimbo mpya wa Chidi Benz, ‘Mpaka Kuchee’ walioshirikishwa.

“Watu wategemee video nzuri ya Chidi Benz,” alisema.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents