Habari
AY awakumbuka Ngwair na Langa kwenye ‘Sijakusahau ya Crème De La Crème
Ambwene Yessayah aka AY hajawasahau Albert Mangwair na Langa Kileo.
Kupitia wimbo wa DJ wa Kenya, Crème De La Crème ‘Sijakusahau’ hitmaker huyo wa Zigo amewakumbuka rappers hao waliotangulia mbele ya haki.
“Naiona sura ya Ngwair na Langa (Tazama anga), Nakumbuka tuliyopanga lakini Mungu alipanga pia, tuliongazana wengine wakadisappear, daima uzuri umenitanda na moyoni nawalilia,” anarap AY.
Ngwair alifariki May 28, 2013 na Langa June 13, 2013.
Pia AY amewakumbuka wazazi wake kwenye wimbo huo ambao wasanii wengine walioshirikishwa ni Prezzo, Bigpin na Ulopa.
Prezzo amemkumbuka baba yake pamoja na aliyekuwa mpenzi wake Goldie wa Nigeria. Usikilize hapo chini.