Burudani

AT adai Rama Dee amemkosea heshima Adam Juma

Msanii wa muziki AT amemchana msanii Rama Dee kwa kuwambia anapaswa awaheshimu watu waliomtangulia.

Hatua hiyo imekuja siku chache baada ya msanii Rama Dee kusema kiwango cha ‘director’ Mkongwe Adam Juma kiko chini ya viwango katika kutayarisha na kutengeneza ‘video’ na kwamba anamtaka ajifunze kutoka kwa Hanscana kauli ambayo ilipigwa na wadau mbalimbali wa muziki.

“Imekuwa desturi kwenye nchi yetu mtu kutomuheshimu mwenzake au nguvu zake, leo unatoka unasema Adam Juma hajui ku-shoot ‘video’, wakati wewe ukipewa ile kamera hata kupiga picha huwezi kujua lakini yule mtu ndiyo amekuja muziki wa Tanzania”. AT alikiambia kipindi cha eNewz cha EATV

Aidha msanii huyo amesema wasanii ndiyo wanaongoza kwa kutokuwa na heshima, hivyo amewataka wasanii wenzake kuwa na heshima kwa watu waliowazidi.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents