Habari

Askofu Gwajima kutembelea Clouds Jumatano hii

Askofu wa Kanisa la Ufufuo na Uzima, Bishop Josephat Gwajima amesema kuwa Jumatano hii atatembelea Clouds Media Group kwajili ya kuwapa pole kwa yaliyotokea hivi karibuni.

Ijumaa iliyopita kituo hicho kilivamiwa na Mkuu wa mkoa wa Dar es salaam, Paul Makonda akiwa na askari wenye mitutu kitendo kilichopingwa na wadau mbalimbali wa habari.

“Kesho Tarehe 22/03/2017 saa nne kamili asubuhi, nitatembelea Ofisi za Clouds Media ili kuwapa pole kwa yaliyotokea.” aliandika mchungaji huyo kupitia ukurasa wake wa Instagram.

Na Emmy Mwaipopo

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents