Burudani
Ariana Grande asitisha safari ya Hispania kwa hofu ya Ebola
Ugonjwa wa Ebola ni tishio kwa kila mtu kwa sasa duniani ndio maana muimbaji wa Marekani Ariana Grande, 21, ameamua kusitisha safari ya Hispania.
Kutokana na hofu hiyo, mrembo huyo aliamua kuelekea Paris na Hispania ataenda hadi mwezi ujao.
Hadi sasa kumekuwepo na kesi nne za Ebola nchini Hispania ambapo hata hivyo wagonjwa wote hawakukutwa na virusi hivyo.