Michezo

Argentina yaongoza orodha ya FIFA ya timu bora duniani

Shirikisho la soka duniani (FIFA) imetoa orodha mpya ya viwango vya ubora wa soka duniani, bado vinara wamesalia kuwa Argentina.

fifa

Mabadiliko haya yamekuja hasa kwa kuzingatia Matokeo ya Mechi za kuwania kutinga Fainali za Kombe la Dunia za Mwaka 2018 huko Urusi.

Tanzania inashika Nafasi ya 144 baada ya kuporomoka nafasi 12. Uganda wao wapo nambari 72 baada ya kushuka nafasi saba, Kenya wamepanda nafasi sita hadi nambari 85 nao Rwanda wamesalia nambari 107.

Ethiopia wamo nafasi ya 126, Malawi 100 na Burundi 138.

Nchi ambayo ipo juu kabisa kwa Bara la Afrika ni Mabingwa wa Afrika Ivory Coast walio nafasi ya 31 wakifuatiwa na Senegal ambao ni wa 32.

Orodha nyingine ya Ubora wa viwango itatolewa Novemba 24.

Haya ni mataifa 10 bora duniani

1.Argentina

2.Ujerumani

3.Brazil

4.Ubelgiji

5.Colombia

6.Chile

7.Ufaransa

8.Ureno

9.Uruguay

10.Uhispania

Mataifa 10 bora Afrika

31 Ivory Coast

32 Senegal

35 Algeria

38 Tunisia

45 Ghana

46 Misri

49 DR Congo

58 Mali

59 Cameroon

Related Articles

Check Also
Close
Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents