Technology

Apple kuja na iPhone za vioo tupu

Kampuni ya Apple imedai kuwa inafanyia kazi toleo jipya la simu za iPhone ambazo zitakuwa za vioo tupu.

iphone-6-concept-nowhereelse-and-martin-hajek-003-1200x573

Akiongea kwenye mkutano wa kila mwaka wa wana hisa wa kampuni hiyo, mwenyekiti mtendaji wa kampuni inayotengeneza umbo la nje la simu hizo, Catcher Technology, Allen Horng alisema simu hizo mwaka 2017 zitakuja na umbo lenye vioo.

Alisema kuwa ili kuzipa uimara simu hizo zitaweka fremu ya chuma na kwamba zitawagharimu sana kuzitengeneza na hivyo bei yake kuwa juu. Toleo la simu hizo litakuwa ni iPhone 8.

Kampuni hiyo inatarajia kuzindua simu mpya za iPhone 7 baadaye mwaka huu japo zinadaiwa kutokuwa tofauti sana na iPhone 6 na 6s.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents