Burudani
Angelina Jolie na Brad Pitt wafunga ndoa
Waigizaji wa Hollywood, Angelina Jolie na Brad Pitt wameripotiwa kufunga ndoa Jumamosi iliyopita katika sherehe ndogo iliyohudhuriwa na familia pamoja na marafiki huko Ufaransa.
BREAKING: Angelina Jolie and Brad Pitt were married Saturday in France, says a spokesman for the couple.
— The Associated Press (@AP) August 28, 2014
Miongoni mwa waliohudhuria harusi yao ni pamoja na watoto wao sita.
Pitt (50) na Jolie (39) walianza uhusiano mwaka 2005 wakati wanafanya kazi ya filamu ya Mr and Mrs Smith, na walianza uchumba mwaka 2012 ikiwa ni miaka saba toka waanze uhusiano. Wamefunga ndoa wakiwa na miaka tisa ya uhusiano.