Michezo
Angel Di Maria asaini mkataba wa miaka mitano Man United
Nyota wa Argentina na kiungo aliyeng’ara kwenye kombe la dunia, Angel di Maria hatimaye amekuwa mchezaji wa Manchester United kwa dau la Pauni Milioni 59.7 kutoka Real Madrid.
Winga huyo wa Argentina amesaini mkataba wa miaka mitano Old Trafford ambao utamfanya apate mshahara wa Pauni Milioni 6.5 kwa mwaka baada ya kodi.
Hiyo itamfanya mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 26 awe nyuma ya nahodha wa United, Wayne Rooney kwa kulipwa mshahara mkubwa.
Makamu Mwenyekiti, Ed Woodward akitia saini mkataba na Di Maria
Angel di Maria akikabidhiwa jezi ya Manchester United na kocha Louis van Gaal