Habari
Amini afiwa na kaka yake aliyekuwa akiishi Afrika Kusini
Muimbaji na mtunzi wa nyimbo, Amini Mwinyimkuu anayefanya vizuri na wimbo wake ‘Asante’ amepata msiba kwa kufiwa na kaka yake wa tatu aitwaye Kipara Mwinyimkuu aliyekuwa akiishi nchini Afrika Kusini.
Amini ameiambia Bongo5 kuwa msiba upo kwao Kinondoni Msisiri na wanafanya taratibu za kuuleta mwili Dar es Salaam.