Habari

Ally Baucha afiwa na baba yake mzazi


Producer mkongwe nchini wa studio za Baucha Records, Ally Baucha, amefiwa na baba yake mzazi usiku wa kuamkia leo.
Leo usiku muda wa saa 6:26, ametutumia ujumbe wa simu unaosema, “Mambo vp…? Nimefiwa na baba mzazi leo usiku huu. Najua wewe ni mtu muhimu kukutaarifu kwanza, nasubiri kuelekea Zanzibar kwa mazishi… Baucha.”
Baucha amesema kifo cha baba yake Mzee Mohamed Yussuf kimetokana na ugonjwa wa ini.
Mzee Yussuf aliyefariki akiwa na umri wa miaka 69,aliwahi kuwa mkuu wa polisi wa wanamaji mkoa wa Mwanza miaka ya 1980 kabla ya kuhamishiwa Zanzibar.
Bongo5 inampa pole Ally Baucha kwa kifo cha baba yake na Mungu amlaze mahali pema Mzee Mohamed Yussuf.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents