Burudani
Alikiba, Redsan, STL, Radio na Weasel kutumbuiza kwenye uwanja wa Nyayo, Kenya July 10
Alikiba ataongoza (headline) show kubwa iliyopewa jina ‘It’s Big’ itakayokutanisha mastaa wengine wa Kenya na Uganda.
Show hiyo itafanyika kwenye uwanja wa Nyayo uliopo jijini Nairobi, Kenya wenye uwezo wa kuchukua watu 30,000, July 10.
Wasanii wengine watakaopanda jukwaani ni Redsan, Stella Mwangi aka STL, Radio and Weasel wa Uganda na wengine.
Hiyo inakuwa show kubwa zaidi kwa Alikiba tangu asaini deal na Sony Music.