Burudani

Alikiba: ‘Mwana’ ilikuwa nifanye na Fally Ipupa lakini tukaogopa, fahamu kilichomwogopesha

Alikiba amefunguka kuwa single yake mpya ya ‘Mwana’ ambayo ilirekodiwa miaka miwili iliyopita, hapo mwanzo alipanga angemshirikisha mwanamuziki wa DRC, Fally Ipupa.

Kiba na ipupa

Kiba amesema mipango hiyo ilikuja kubadilika baada ya kugundua ngoma imekuwa kali bila Fally hivyo ikamlazimu kuiacha kama ilivyo na kuandaa wimbo mwingine atakaomshirikisha star huyo.

“(Mwana) ilikuwa nifanye na Fally before, lakini sasa tulipoona nyimbo nimerekodi ikwa nzuri zaidi tukasema tusiiharibu anaweza akarekodi labda bahati mbaya ameharibu bahati mbaya amepatia kwahiyo nikamwandalia ngoma nyingine Fally,” amesema Alikiba kupitia XXL ya Clouds FM.

“kwahiyo ilikuwa imeandaliwa beat lakini sasa kwa utamu nilivyokuwa nimeuzidisha sana mle ndani mpaka tukaogopa kwamba Fally asije akapotea au akapoteza zaidi, lakini sikufikiria hilo, kitu cha muhimu ambacho nilifikiria kwamba ukiona nyimbo imekuwa nzuri zaidi sana, iache hivyo hivyo iende tutafute kingine.”

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents