Burudani

Alikiba awajibu wanaodai video ya ‘Mwana’ ni mbovu

Hatimaye Alikiba ameamua kuwajibu baadhi ya wapenzi wa muziki walioikosoa video ya wimbo wa ‘Mwana’ wanaodai kuwa haiendani na kile kinachoimbwa.

Akizungumza na 255 ya XXL ndani ya Clouds FM, Alikiba amesema alichokifanya alimaanisha hivyo kuleta picha mpya kwenye vichwa vya watu.

“Utofauti wa video ndio uzuri wake kwa sababu kila mtu kwenye mind yake amejenga video, ame-create video itakuwa vipi,” amesema. Kwa sababu nyimbo imeelezea vitu vingi ni pana kama unavyoona na ina vitu vingi madawa, ma-prostitute, ukabaji, wizi, vitu fulani vingi sana nisingeweza vyote kuweka katika video kwa sababu kila mtu anamind yake. Kwahiyo nilivyofanya utofauti nili-concetrate kwenye dancing na kucheza na feeling za kuimba. Video nyingi zimeshafanyika duniani sio ya kwangu tu, kwahiyo watu wasishangae vitendo havikuwepo nimemaanisha sio nimefanya ili tu nitoe video.”

“Ule utofauti uliokuwepo ndo uzuri wa video yenyewe. Professionals walifanya hiyo video kwa sababu ni production kubwa iko na watu ambao wali script vile vile kwahiyo tulishauriana na tuka appreciate kufanya hicho kitu. Dancing style inaitwa Kalila. Choreographer wangu ndio alifanya hiyo yote kila kitu.”

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents