Burudani

Alikiba akanusha kuandaa watu wamzomee Diamond kwenye Fiesta

Alikiba amekanusha uvumi unaodai kuwa huenda aliaandaa watu maalum wa kumzomea Diamond Platnumz kwenye show ya Fiesta iliyofanyika October 18 katika viwanja vya Leaders Club jijini Dar es Salaam.

Ali Kiba akiwa kwenye pozi ndani ya jukwaa la fiesta Dodoma

Alikiba ameiambia Bongo5 kuwa hajui uvumi huo umeanza vipi.

“Hamna ukweli wowote, naanzaje?,” amehoji. “Siwezi kufanya kitu kama hicho. Kikubwa ni kuwashukuru wana Dar es Salaam walivyonipokea, nimefurahi sana. Hii imenitia moyo na kunifanya niongeze bidii kuwaandalia vitu vizuri zaidi.”

Katika hatua nyingine, msanii huyo amesema mashabiki wa muziki wake wasishangae kuona video ya wimbo wa ‘Mwana’ wiki hii ama wiki ijayo. “Video ni muda wowote yaani, usishangae ukasikia video imetoka. Muda wowote video inatoka surprise, kwahiyo waendelee kusubiri muda wowote.”

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents