Burudani
Ali Choki kupunguza urefu wa nyimbo za bendi yake, adai ni kuendana na mahitaji ya soko
Kiongozi wa bendi ya Extra Bongo, Ali Choki amesema kuanzia album yake ijayo, nyimbo za bendi hiyo zitakuwa fupi.
Akiongea na TBC One, Choki amesema wamebaini kuwa soko la sasa halihitaji nyimbo ndefu zinazoonesha kuwachosha watu. Nyimbo nyingi za dance huwa na dakika kuanzia 8 hadi 12 au na zaidi wakati nyimbo za Bongo Flava huanzia dakika 4 hadi 4 au 5.
Katika hatua nyingine bendi hiyo inayotarajia kuanza ziara ya nchi nzima, imemrejesha kundi muimbaji mkongwe, Banza Stone.