Burudani

Album ya Flavour ‘Thankful’ yauza kopi milioni 1 ndani ya siku 5!

Album mpya ya msanii wa Nigeria, Flavour iitwayo Thankful iliyotoka November 14, imeuza kopi milioni moja hadi sasa, kwa mujibu wa mitandao ya Nigeria.

Untitled

Album hiyo ilitoka bila promo wala matangazo yoyote, kama alivyofanya Beyonce.

Kwa mujibu wa kampuni ya Obaino Music, inayohusika katika uuzaji wa album hiyo yenye nyimbo 21, hadi jana Jumatano walikuwa wameshauza kopi milioni 1 za kwanza. Kampuni hiyo imesema kwa jinsi msanii huyo anavyopendwa, album hiyo itauza kopi nyingi zaidi.

Album hiyo imewashirikisha wasanii mbalimbali wakiwemo M.I, Phyno, Wande Coal na Chidinma.

Related Articles

Leave a Reply

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents