Burudani
Album mpya ya Rihanna ‘ANTI’ itapatikana exclusive kwa wiki moja kwenye Tidal
Kuna tetesi kuwa album mpya na ya nane ya Rihanna, ANTI itatoka Ijumaa hii na kupatikana kwenye mtandao wa Tidal peke yake kwa kipindi cha wiki moja kabla ya kuwekwa kwingine.
Billboard wamedai kuwa hatua hiyo itaathiri mauzo ya wiki ya album hiyo. Rihanna ni miongoni mwa mastaa wenye hisa kwenye mtandao wa Tidal.
Hata hivyo kazi nyingi zilizowekwa kwenye mtandao huo zimeonesha kutokuwa na mapokezi makubwa kama zinazowekwa kwenye Spotify na YouTube.
Mfano mzuri ni wimbo wake ‘American Oxygen’ iliyotoka kupitia Tidal ambao haukufanya vizuri ilivyotegemewa.