Ajali ya Zong Hua Garden
Wakati natoka X BONGO NITE, pale New Maisha club yapata kama saa kumi na nusu hivi usiku wa mach 21, ndipo nikakutana na ajali maeneo ya barabara ya Morocco karibu na Zong Hua Garden, ajali ambayo ilisababishwa na mwenye pikipiki (Kwa mujibu wa mabishano ya Trafki na dereva wa pikipiki, kwa lengo la kutaka kupima ilikuhakiki) huku dreva wa pikipiki akionekana kama ambaye ameonja kidogo.
Ajali hiyo ilikuwa ya gali aina ya Land Cluiser na pikipiki (Toleo la mchina aka Bodaboda), lakini hadi naondoka pale sikuwa na uhakika kama kuna mtu yoyote aliyejeruhiwa, na kukimbizwa hospitali kwani maongezi yalikuwa yakibezi sana na mwenye pikipiki ambaye alionekana kuchanganyikiwa zaidi.