Burudani
Afande Sele azungumzia ujio wa nyimbo mbili mpya
Afande Sele anatarajia kuachia nyimbo mbili kwa mpigo.
Rapper huyo ameiambia Bongo5 kuwa uamuzi wa kuachia nyimbo mbili ni kukata kiu ya mashabiki wake waliokuwa wakisubiria muziki wake.
“Kuna nyimbo mbili bado zipo kwenye maandalizi, moja inaitwa Mfungwa. Hii ni nyimbo ambayo ndani nitazungumzia matatizo yanayowakuta wafungwa, wafungwa wanavyonyanyasika,” amesema Afande.
“Na wimbo wa pili utazungumzia pia maisha fulani jinsi tunavyoishi kwa visasi, unakuta dereva wa gari ana kisasi na muuza mafuta, muuza genge ana kisasi na muuza nyanya. Kwahiyo ni wimbo fulani ambao utahitaji kutuweka sawa ili kuishi kwa pamoja bila kuwa na visasi.”