Habari
Adam Mchomvu kuzindua video yake mpya Jumapili hii Club Bilz
Mtangazaji mahiri wa kipindi cha XXL na Bongo Flava vya Clouds FM ambaye pia ni rapper, Adam Mchomvu atazindua video ya wimbo wake mpya uitwao ‘Tiririka’ Jumapili hii.
Uzinduzi huo utafanyika kama sehemu ya tamasha la ‘Vitu Fulani Amazing’ Club Bilz zamani Billicanas jijini Dar.
Mchomvu atasindikizwa na wasanii kibao wakiwemo Joh Makini, Nick wa Pili, Young D, Jay Moe, Roma, Belle 9, Shilole, Stereo, Kigogo T.I.D. na surprises za wasanii wakubwa Tanzania..
Director wa video hiyo ni Hanscana.
Hii ndo show kubwa zaidi ya Bongo fleva ndani ya club hiyo kwa mwaka huu na Mchomvu ndiye msanii wa kwanza kufanya show ndani ya Bilz mpya.