Michezo
Abou Diaby kurudi uwanjani baada ya miezi 17 kuwa nnje
Mchezaji wazamani klabu ya Arsenal Abou Diaby ambaye alikuwa kila mara majeruhi sasa amerudi. Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 29 anatarajiwa kurudi uwanjani akiichezea Marsaile baada ya miezi 17 ya kuuguza jereha.
Diaby ambaye alicheza mechi mbili katika msimu wake wa mwisho na kilabu ya Arsenal aliachwa na kilabu hiyo katika msimu wa joto.
Bahati yake mbaya imeendelea katika taifa lake la Ufaransa baada kupata jereha akiwa zoezini, lakini sasa anatarajiwa kurudi katika mechi ya kombe la Ufaransa dhidi ya Trelissac siku ya Alhamisi.