Burudani
50 Cent akiri utajiri anaouonyesha mitandaoni ni feki
Mastaa wa Marekani waliotikisa kwa utajiri miaka kadhaa wameonekana kukumbwa na wimbi la kufilisika hasa wanapotakiwa kulipa madeni wanayodaiwa.
Msanii kutoka nchini marekani, Curtis Jackson maarufu kama 50 Cent, amesema mali zote zinazoonekana mitandaoni zikiwemo pesa, nyumba inayosemekana ipo Afrika n.k, hivyo vyote ni feki havina ukweli wowote.
Siku chache zilizopita, Judge Ann Nevins alimuamuru 50 Cent kulipa dola milioni tano, pesa hizo anatakiwa kulipwa msichana ambaye 50 Cent alituma video ya uchi ya msichana huyo mtandaoni bila ya kupata idhini yake.
50 Cent amekata rufaa kuhusu kulipa pesa hizo ambazo zinaonekana kuwa ni kiasi kikubwa sana kwake.