Burudani
2 Chainz kutumbuiza Kenya mwezi ujao
Afrika Mashariki inatarajiwa kuwa na ugeni wa mastaa wa hip hop nchini Marekani mwezi huu na ujao.
Wakati T.I. akitarajiwa kutumbuiza jijini Dar October 18, rapper 2 Chainz atatua jijini Nairobi, Kenya mwezi ujao.
Rapper huyo ambaye jina lake ni Tauheed Epps atatumbuiza November 1 kwenye Ngong Racecourse. Wasanii wa Kenya watakaotumbuiza ni pamoja na Kaligraph Jones na Kristoff.